TUME YA MADINI

CONTACT US | FAQs | STAFF MAIL | ENGLISH / SWAHILI

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF MINERALS

 THE MINING COMMISSION

Uncategorized

MCHIMBAJI MDOGO WA DHAHABU AMPA TANO RAIS DKT. SAMIA

SERIKALI ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wachimbaji wadogo wa madini kuhakikisha wanapata mitaji, leseni na matumizi ya teknolojia katika shughuli za uchimbaji wa madini na kuwezesha kuchimba kisasa. Akizungumza katika mahojiano maalum mmiliki wa Mgodi wa Kwasakwasa uliopo kijiji cha Msesule kata ya Mapogoro, wilayani Mbarali mkoani Mbeya, mwanadada Amagite Mkumbwike amesema, Serikali ya Awamu ya Sita imeweka mazingira wezeshi ikiwemo bei nzuri sokoni ili wachimbaji wadogo waweze kunufaika zaidi. “Nikiwa mchimbaji mdogo na mmiliki wa mgodi wa Kwasakwasa, nitaendelea kumuunga mkono Rais Samia kwa kuendelea kutoa ajira kwa vijana na kurudisha faida kwa kile kinachopatikana katika vijiji vinavyozunguka mgodi wetu,”amesema na kuongeza, “Serikali imerahisisha vitu vingi ikiwemo kuhakikisha bei ya dhahabu sokoni zinakuwa juu ili wachimbaji wadogo tunufaike. Tumeendelea kuunga mkono jitihada hizo kwa kurudisha faida kwa jamii ikiwemo kununua vifaa vya shule kwa wanafunzi wa kijiji hiki ambao wameendelea na masomo yao ya elimu ya juu, pamoja na kununua mashine ya umwagiliaji hapa kijijini,”amesema Amagite Aidha, kwa upande wa Msimamizi wa Mgodi huo Edward Daud ameiomba Serikali kuendelea kuweka mazingira rafiki zaidi kwa wawekezaji ili vijana wengi wapate ajira kutokana na uwekezaji unaofanywa. “Na sisi vijana tunapoaminiwa sehemu yoyote ile tukapewa kazi basi tuifanye kwa bidii kwa asilimia 100, tuwe waaminifu kwa waliotupa dhamana,”amesema.

MCHIMBAJI MDOGO WA DHAHABU AMPA TANO RAIS DKT. SAMIA Read More »

KIKAO CHA TUME YA MADINI CHAWEKA MIKAKATI YA KUINUA SEKTA YA MADINI

  Dodoma Leo Februari 11, 2025 Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Janet R. Lekashingo ameongoza kikao cha Kamisheni ya Tume ya Madini kilichofanyika jijini Dodoma kwa lengo la kupokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya Tume ya Madini kwa kipindi cha miezi mitatu sambamba na kuweka mikakati ya kuhakikisha Sekta ya Madini inaendelea kuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi. Kikao hicho kilichoshirikisha Makamishna wa Tume na Menejimenti kimeendelea kuweka mikakati mipya ya kuhakikisha Sekta ya Madini inaendelea kuwa na mchango kwenye Pato la Taifa kupitia uboreshaji wa usimamizi kwenye shughuli za uchimbaji na biashara ya madini, ukusanyaji wa maduhuli na masoko ya madini na udhibiti wa utoroshaji wa madini. Akielezea mafanikio ya Tume ya Madini tangu kuanzishwa kwake, Katibu Mtendaji wake, Mhandisi Ramadhani Lwamo ameeleza kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa 30 katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na Ofisi za Maafisa Migodi 13 kwa Migodi Mikubwa na baadhi ya Kati; Masoko ya Madini 43 na Vituo vya Ununuzi wa Madini 108. Ameeleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na Uboreshaji wa Huduma za Maabara kwa Wachimbaji na Wafanyabiashara wa Madini; Uwepo wa mifumo thabiti ya kieletroniki ya ukusanyaji wa mapato pamoja na utoaji wa leseni; Ushirikiano thabiti wa ndani na nje ya Tume ya Madini dhidi ya Mamlaka nyingine za Serikali na kuendelea kukua kwa kasi ya ukusanyaji wa maduhuli ya Serikali na maboresho ya Sheria, Kanuni na Taratibu na miongozo inayosimamia Sekta ya Madini. Akizungumza kwenye kikao hicho Mwenyekiti wake, Janet Lekashingo amepongeza kazi nzuri inayofanywa na Tume ya Madini hasa kwenye eneo la ukusanyaji wa maduhuli, usimamizi wa masoko ya madini na vituo vya ununuzi wa madini vilivyoanzishwa nchini, kuimarika kwa usalama kwenye shughuli za uchimbaji wa madini, ushirikishwaji wa watanzania katika Sekta ya Madini na mchango wa kampuni za madini kwa Jamii. Kupitia kikao hicho mikakati mbalimbali imewekwa kupitia Kamati za Ufundi, Rasilimaliwatu, Fedha na Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini.

KIKAO CHA TUME YA MADINI CHAWEKA MIKAKATI YA KUINUA SEKTA YA MADINI Read More »

MADINI YA VIWANDA, DHAHABU NA MADINI UJENZI YAPAISHA MKOA WA MBEYA

· Yafikia asilimia 63 ya lengo la Mwaka la makusanyo · Waita wawekezaji MAKUSANYO ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Mbeya yatokanayo na mrabaha, tozo na ada mbalimbali, kwa mwaka wa fedha ulioanza Julai 2024/ 2025 jumla ya Shilingi Bilioni 2.3 zilikusanywa ikiwa ni sawa na asilimia 63 ya lengo la mwaka. Makusanyo hayo ni sawa na asilimia 108 ya lengo la kipindi cha miezi saba (Julai, 2024 mpaka Januari, 2025). Akizungumza kwa niaba ya Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Mbeya, Mhandisi Migodi, William Kajumla amesema Mkoa wa Mbeya ulipangiwa kukusanya Shilingi Bilioni 3.7. Amesema, mapato makubwa katika Mkoa wa Mbeya yanatokana na madini ya viwandani, dhahabu na madini ujenzi, pamoja na mapato katika miradi mbalimbali ya barabara. “Tunategemea mapato kutoka kwenye kiwanda kinachozalisha hewa ya ukaa cha TOL Gas Rungwe, na Kiwanda cha Saruji ‘Mbeya Cement’ kwa madini ya viwandani lakini pia biashara ya dhahabu na machimbo madogo madogo ya madini ujenzi,”amesisitiza. Aidha, Mhandisi Kajumla ametoa wito kwa watanzania kuchangamkia fursa za uwekezaji zilizopo katika Mkoa wa Mbeya hususan sekta ya madini ujenzi, makaa ya mawe Ngana Kyela na Rungwe na fursa za uwekezaji kwenye uchimbaji na uchenjuaji wa dhahabu kwenye maeneo ya Mabadaga, Msesule na Madibira Wilayani Mbarali na Lwanjiro, Ileya, Ishinda na Chikula Wilayani Mbeya.  

MADINI YA VIWANDA, DHAHABU NA MADINI UJENZI YAPAISHA MKOA WA MBEYA Read More »

WATUMISHI MADINI WAASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII, KUWA WAZALENDO

– Watakiwa kuongeza bidii kufikia asilimia 10 mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa – Watakiwa kulinda afya, kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukiza WATUMISHI wa Wizara ya Madini na Taasisi zake wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na uzalendo ili kulinda uchumi wa nchi usiweze kuathirika na mabadiliko ya sera za mataifa ya nje. Akizungumza leo Februari 8, 2025 katika Bonaza lililoandaliwa na Tume ya Madini na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), lililofanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlin jijini Dodoma, Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa amesema Tanzania ina kila aina ya rasilimali ni vyema kuzitunza, kuzithamini na kutanguliza uzalendo mbele ili uchumi wa nchi uendelee kuwa imara. “Nchi za Falme za Kiarabu wametajirika kwa rasilimali moja tu ya uchimbaji mafuta, sisi tuna kila kitu, madini ambayo tumepewa dhamana kubwa ya kusimamia tufanye kazi kubwa kama timu kwa ushirikiano, amesema Naibu Waziri Kiruswa. Amesema, ili kufikia lengo la asilimia 10 ambalo Sekta ya Madini inapaswa kuchangia katika Pato la Taifa ni lazima kufunga mkanda. “Tunapaswa kufunga mkanda ili kufikia lengo la asilimia 10, siku zilizobaki si nyingi ingawa tumepiga hatua kiasi kikubwa,”amesema, Mhe. Dkt. Kiruswa. Awali akizungumza Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba amewataka watumishi kuendelea kuwa wazalendo na kufanya kazi kwa bidii na kujituma, ili Sekta ya Madini iwe na mchango mkubwa katika taifa na kuleta unafuu kwa wananchi. Naye Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Janet Lekashingo amewasihi watumishi katika Sekta ya Madini kutunza afya kwa kufanya mazoezi ili kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukiza. Aidha, Lekashingo amekabidhi tuzo maalum kwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwamo kutokana na utendaji wake uliotukuka, busara zake na ukarimu wake na kuaminiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye Januari 15, 2025 alimthibitisha rasmi kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini. Wakati huohuo Naibu Waziri Kiruswa ametoa tuzo na zawadi mbali mbali kwa viongozi wastaafu ikiwa ni pamoja na kuwaaga rasmi aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula na Profesa Abdulkarim Mruma aliyekuwa Kamishna wa Tume ya Madini. Katika hatua nyingine washindi wa michezo mbalimbali wamekabidhiwa vikombe na medani Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Madini ni Tume ya Madini, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST), Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) na Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI)

WATUMISHI MADINI WAASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII, KUWA WAZALENDO Read More »

IRINGA FURSA ZA MADINI ZIPO NJOONI – MHANDISI MILANDU

Yakaribia 60% ya lengo ukusanyaji maduhuli kwa mwaka 2024/2025 Yaita wawekezaji wakubwa kuwekeza Sekta ya Madini MAKUSANYO ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Iringa yatokanayo na mrahaba, tozo na ada mbalimbali kwa mwaka wa fedha 2024/2025 yamefikia shilingi milioni 698.05 ikiwa ni asilimia 58.2 ya lengo walilowekewa. Akizungumza katika mahojiano maalum, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Iringa, Mhandisi AbdulRahman Milandu amesema Mkoa wa Iringa umewekewa lengo la kukusanya Shilingi Bilioni 1.2. “Mwaka huu wa fedha mpaka sasa tunakaribia asilimia 60, tumekusanya shilingi milioni 698.05 zaidi ya nusu ya lengo, hii inaonyesha fursa zipo,” amesema na kuongeza, Aidha, Mhandisi Milandu ametoa wito kwa wawekezaji wote nchini kuchangamkia fursa za uwekezaji zilizopo katika Sekta ya Madini mkoani Iringa ambapo mkoa huo umebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali ikiwemo dhahabu, vito, chuma, madini ya viwandani na madini ya ujenzi. “Madini ujenzi yapo tele wawekezaji waje kuwekeza, pia tuna maeneo ya dhahabu kama Nyakavangala, Ifunda, Kitengulinyi, kijiji cha Sinai na Igoma Wilayani Mufundi yana fursa ya madini ya kutosha ya dhahabu hivyo wawekezaji wakubwa waje kuwekeza,”amesisitiza.

IRINGA FURSA ZA MADINI ZIPO NJOONI – MHANDISI MILANDU Read More »

INCREASED USE OF EXPLOSIVES IN TANZANIA SPARKS CALL FOR STRICTER REGULATIONS

Dodoma, January 13, 2025 The use of explosives in Tanzania has surged dramatically, rising from an average of 3,000 tons annually in the 1990s to 26,516.07 tons in 2024, a trend attributed to the expansion of mining, oil and gas exploration, and infrastructure projects. This was highlighted today by Engineer Ramadhani Lwamo, Acting Executive Secretary for the Mining Commission, during a session aimed at strengthening the capacity of mine and explosives inspectors in Dodoma. “The growing use of explosives underscores the increase in mining activities across the country. However, without proper oversight, this could result in catastrophic consequences,” Engineer Lwamo cautioned. He emphasized the urgent need for strict regulation to prevent accidents, noting, “This session is designed to empower inspectors to ensure miners’ safety and prevent injuries stemming from explosive misuse. Inspectors must take control of their regions to avoid tragedies that could tarnish the industry.” The session also revealed that Tanzania currently has over 231 magazines, 493 storage facilities, and 279 registered explosive storage boxes in use, underscoring the widespread nature of the explosives trade. Engineer Hamisi Kamando, Acting Mines Inspectorate and Environment Director, highlighted the dangers associated with non-compliance with existing laws, including the Explosives Act of 1963 and the Explosives Regulations of 1964. “Several accidents could have been prevented with proper adherence to the laws,” he said. In support, Senior Legal Officer Damian Kaseko urged inspectors to remain vigilant and adhere strictly to laws, policies, and regulations to avoid legal conflicts and ensure clarity in their roles. The growing demand for explosives has opened opportunities in Tanzania but has also introduced risks that necessitate robust oversight. As officials and stakeholders work to address these challenges, the focus remains on ensuring safety and minimizing harm in the burgeoning sector.

INCREASED USE OF EXPLOSIVES IN TANZANIA SPARKS CALL FOR STRICTER REGULATIONS Read More »

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA ITALIA KUENDELEZA SEKTA YA MADINI

▪️Mkutano wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Italia kufanyika Mwezi Februari, 2025. ▪️Kampuni za Utengenezaji Vifaa kutoka vya Madini kutoka Italia kushiriki. ▪️Wachimbaji kunufaika na teknolojia na mitambo rafiki kwa mazingira 📍Dar es Salaam Waziri wa Madini, Mh. Anthony Mavunde (Mb) amesena kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na Italia katika kuendeleza sekta ya madini nchini hususani katika teknolojia na mitambo. Ameyasema hayo jana tarehe 06 Januari, 2025 alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mh. Giuseppe Coppola katika ofisi ndogo za Wizara ya Madini Jijini Dar es Salaam. “Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameifungua nchi yetu kwa kuimarisha mahusiano kimataifa kupitia falsafa yake ya 4R. Sisi wasaidizi wake tutaendelea kuhakikisha tunasimamia maono hayo na kujenga mahusiano zaidi na washirika wetu kwa manufaa ya uchumi na wananchi wa pande zote. Zipo fursa nyingi kwenye sekta ya madini nchini kuanzia kwenye utafiti mpaka uongezaji thamani madini, mazingira ya uwekezaji ni mazuri hivyo ninawakaribisha sana wawekezaji kutoka nchini Italia kuja kuwekeza Tanzania“alisema Mavunde. Kwa upande wake Balozi Coppola, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano inaompa tangu awasili nchini, na kusisitiza kwamba Italia inayo makampuni mengi ambayo yamejikita katika teknolojia hususan utengenezaji wa mitambo inayotumika kwenye sekta ya madini. “Mwezi Februari, 2025 tunataraji kuwa na mkutano wa wafanyabiashara baina ya Tanzania na Italia ambapo tunatarajia makampuni na wawekezaji katika sekta zote hususan madini kuja kushiriki mkutano huo. Ninaamini kwa kutumia mkutano huo utakuwa ni mwanzo mzuri wa wawekezaji kutoka Italia kuona fursa zilizopo nchini Tanzania na kuanza kuzichangamkia” alisisitiza Mhe. Coppola. Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde alionesha kufurahishwa na mpango wa mkutano wa wafanyabiashara wa Italia na Tanzania na kutanabaisha kwamba ni vizuri taarifa za kina kuhusu mkutano huo zikaifikia Wizara mapema kwa ajili ya uratibu ili wachimbaji wakubwa na wadogo waweze kushiriki kikamilifu na kuleta tija.

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA ITALIA KUENDELEZA SEKTA YA MADINI Read More »

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI YA KUREJESHA HADHI YA MADINI YA TANZANITE

-Waziri Mavunde azindua mnada wa ndani Mirerani leo. – Minada ya ndani na nje ya nchi kutumika kutangaza madini ya vito. -Madini yote yatakayokosa wanunuzi kurejeshwa kwa wahusika -Wadau waonesha nia ya kujenga Mji wa Kimadini Mirerani Mirerani MANYARA: Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde amesema Serikali imejidhatiti kurudisha hadhi ya Tanzanite kwa kufanya minada ndani na nje ya nchi ili kuyaongezea thamani na wafanyabiashara waweze kunufaika na kuongeza pato la taifa kwa ujumla. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Desemba 14, 2024 Mirerani mkoani Manyara wakati akizindua mnada wa madini ya vito ambao mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2017. Mheshimiwa Mavunde amesema mojawapo ya maeneo yanayosaidia kuongeza mapato ni pamoja na kudhibiti biashara ya madini, kuzuia utoroshaji na kuifanya biashara hiyo kuwa katika mfumo sahihi, uwepo wa minada utachochea uongezaji thamani ya madini ya vito. “Madini ya Vito yananunuliwa kwa asilimia kubwa kwa ajili ya ‘luxury’ ni ufahari na madini ya vito tunashindana na watu wengine ndio maana Serikali inaendelea kuchukua hatua, tunarudisha hadhi ya Tanzanite ili ikashindane vizuri duniani,”amesema Waziri Mheshimiwa Mavunde na kuongeza, “Moja ya hatua ya kwanza ni urejeshaji wa minada ya ndani na ya kimataifa, ili tuyape thamani madini yetu, duniani kuna madini mengi ya vito, moja ya sifa kubwa ya madini ya vito ni uadimu, Tanzanite ina sifa hizo; Ila sio madini pekee yake adimu, kuna nchi nyingine zina madini adimu ambayo hayapatikani popote hivyo tunashindana kimataifa ni lazima tuchukue hatua kuhakikisha tunarudisha hadhi ya Tanzanite katika soko la kimataifa ili na bei iweze kuongezeka na wafanyabiashara wanufaike,”amesisitiza Waziri Mavunde Amesema, katika vipengele (category) vya mawe duniani, jiwe linaanzia kuwa Precious, semi-Precious halafu baadaye linakuwa jiwe la kawaida na kwamba wanachukua hatua za makusudi ili Tanzanite lisiwe jiwe la kawaida. “Tukiacha liwe la kawaida mtanunua kwa kilo kwa gharama ndogo sana na mtashusha hadhi ya Tanzanite, Serikali haipo tayari kuona hilo linatokea ndio maana tunayafanya haya kwa ajili ya kuhakikisha tunalinda hadhi na heshima ya jiwe letu hili.” Amesisitiza Mheshimiwa Mavunde. Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde amewahakikishia wadau wa madini kuwa Serikali haitachukua madini ya mtu baada ya mnada wa leo na kama kuna madini yatabaki yatakabidhiwa kwa wahusika. “Kumekuwepo na hisia na dhana baada ya mnada Serikali itachukua madini yaliyobaki kwa sababu katika mnada wa mwisho wa mwaka 2017 kuna madini yalibaki na wahusika hawakurejeshewa mpaka leo, nataka niwahakikishie Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kusimamia kuhakikisha katika biashara hii pia tuwajengee ‘confidence’ mtafanye biashara kwa uhuru na hakuna namna yoyote kuwa serikali itawaingilia na kuja kuyachukua madini yenu. “Yale madini yaliyochukuliwa yapo, yalibaki Benki Kuu ya Tanzania (BoT) tumeshayatoa na tutawakabidhi rasmi wahusika ili waendelee na biashara yao ya madini, nataka niwatoe hofu na muwe na amani,”amesema Waziri Mavunde. “Manyara tayari mna eneo ambalo tutajenga ‘Tanzanite Exchange Centre’ ambayo kwa sasa tumefanya mazungumzo na wadau tutajenga kitu kinaitwa ‘Tanzanite Smart City’ ambao utakuwa mji mkubwa wenye hoteli ndani yake, Helikopta ambazo zitatua humo humo, ukumbi mkubwa wa mikutano wahusika hivi sasa wapo Wizara ya fedha, likikamilika hili natamani siku moja mkutano mkubwa wa madini ufanyike Mirerani.”Amesema. Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo ameongeza kuwa kupitia mnada huu uliozinduliwa leo, idadi ya wauzaji waliojisajili kwenye mfumo wa kielektroniki wa kuendesha minada ni 195 wakiwemo wafanyabiashara wadogo wa madini (brokers) 120, wafanyabiashara wakubwa wa madini (dealers) 59, waongeza thamani madini (lapidary) 7 na wachimbaji madini 9. Kiasi cha madini kilicholetwa kwenye mnada ni kilogramu 184.06 kinachokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi za kitanzania bilioni 3.10. Wakati huohuo akizungumza kwenye uzinduzi wa mnada huo Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda amempongeza Waziri wa Madini kwa kuweka nguvu kubwa kwenye utafiti wa madini kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na kuwezesha wachimbaji kuchimba bila kupoteza mitaji ikiwa ni sehemu ya “Vision 2030 ya Madini ni Maisha na Utajiri,” na kuongeza kuwa, “Kamati itaendelea kutoa ushirikiano kwa Wizara lengo likiwa ni kuhakikisha mchango wa Sekta ya Madini unakua na kufikia asilimia 10 ifikapo mwaka 2025” Naye Mbunge wa Simanjiro Mheshimiwa Christopher Ole Sendeka amepongeza jitihada za Serikali kwa kupania kuleta mapinduzi ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa masoko na vituo vya ununuzi wa madini nchini, kuhakikisha dhahabu inanunuliwa kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hivyo kuendelea kuimarisha uchumi wa nchi. “Ninashauri Serikali kuendelea kutilia mkazo wa biashara ya madini ya vito kuendelea kufanyika katika mji wa Mirerani wakati ujenzi wa Soko la Madini Mirerani ukiendelea” amesisitiza. Naye Mkuu wa Mkoa wa Manyara , Mheshimiwa Queen Sendiga ameongeza kuwa minada ya madini ya vito italeta manufaa makubwa kwa nchi ikiwa ni pamoja na kukuza kipato kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini, serikali kupata mapato, kuimarisha ubora wa madini ya vito na kuongeza ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini na kuwataka wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini.

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI YA KUREJESHA HADHI YA MADINI YA TANZANITE Read More »

COMPREHENSIVE STRATEGIES SET TO BOOST THE MINERAL SECTOR

Dodoma Today, December 5, 2024, the first meeting of the new Commision for the Mining Commission was held in Dodoma, following the appointment of the new Chairperson of the Mining Commission, Janet Reuben Lekashingo. The meeting brought together Commissioners of the Commission and the Management Team to receive and discuss the quarterly implementation report of the Commission’s duties. Speaking at the meeting, the Chairperson, Janet Lekashingo, commended the Mining Commission for its excellent work, particularly in revenue collection, managing mineral markets and buying centers established in the country, enhancing safety in mining activities, local content and corporate social responsibility During the meeting, various strategies were outlined through the Technical, Human Resources, Financial, and Local Content Committees to further develop the sector.

COMPREHENSIVE STRATEGIES SET TO BOOST THE MINERAL SECTOR Read More »

KURUDI KWA MINADA YA MADINI MIRERANI KUTASAIDIA KUONGEZA THAMANI YA MADINI – WADAU MADINI

🔹️ Biashara kufanyika kidijitali kupitia Soko la Bidhaa Tanzania-TMX 🔹️ Waziri Mavunde kuwa Mgeni Rasmi Hafla ya Mnada 🔹️ Wanawake wahamasishwa kuchangamkia fursa za biashara katika mnyororo wa madini_ 📍 Mirerani- Manyara Wafanyabiashara wa Madini nchini Tanzania wameelezea matumaini yao makubwa kuhusu hatua ya kurejeshwa kwa Minada ya Madini katika eneo Mirerani, Mkoa wa Manyara na kueleza kuwa kurejea kwa minada hiyo kutasaidia kuleta mchango mkubwa katika kuongeza thamani ya madini, hususan Tanzanite, ambayo ni madini adimu yanayopatikana nchini Tanzania pekee. Hayo yameelezwa kwa nyakati tofauti na baadhi ya wafanyabiashara wakati wakizungumza na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Madini leo Desemba 13, 2024 kuelekea Siku ya Mnada wa Madini ya Vito Mirerani 2024 inayotarajiwa kufanyika Desemba 14, 2024. Wafanyabiashara hao wameitaka Serikali kuendelea kushirikiana na wadau ili kuhakikisha kuwa minada inafanyika mara kwa mara, kwa uwazi, na kwa misingi ya haki, ili kutoa faida kwa pande zote zinazohusika. Kwa pamoja, wanatarajia kuwa kurudi kwa minada ya madini Mirerani kutakuwa ni hatua muhimu ya kuimarisha thamani ya madini ya Tanzania na kukuza uchumi wa taifa. Akizungumzia Mnada huo, Mfanyabiashara wa Madini (Dealer) Upendo Kibona ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Lucid Dream Limited amesema kuwa kurejea kwa minada ya madini Mirerani itaongeza uwazi katika soko la madini na kuhakikisha kuwa wauzaji wanapata bei stahiki kutokana na ushindani wa moja kwa moja kati ya wanunuzi. “Kwa kweli tunaishukuru sana Serikali kwa kurejesha minada hii, kwasababu inatupa fursa ya kuuza madini yetu kwa bei ya ushindani, pamoja na kuwa huu ni mnada wa ndani lakini utasaidia kuongeza ushindani katika bei, na hata hiyo minada ya kimataifa itakapoanza nadhani tutakuwa sehemu nzuri zaidi” amesema Kibona. Kwa upande wake, Broker wa Madini Glory Robinson amesema, matarajio yake ni kuona minada hiyo inachochea uchumi wa ndani kupitia ajira na biashara ndogo ndogo zinazotegemea shughuli za madini na kwamba Mirerani inaweza kuwa kitovu cha maendeleo ya kiuchumi kwa Mkoa wa Manyara, kwa kuwa minada huvutia wanunuzi wa ndani na nje ya nchi, ambao pia hutumia huduma za hoteli, usafiri, na bidhaa nyingine za ndani. “Niwahamasishe wanawake wenzangu kuchangamkia hii fursa, kwa sababu kupitia biashara zilizopo kwenye mnyororo mzima wa shughuli za madini zinaweza kuwasaidia kuinua vipato vyao na kuendesha maisha yao sambamba na kutunza Familia zao” amesisitiza Glory. Naye, Broker wa Madini Sweety Nkya, amesema kuwa Serikali imeonyesha dhamira ya kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mkubwa zaidi kwa pato la taifa ambako kupitia mifumo hiyo ya Minada, biashara itafanyika kwa haki na washindi watapata haki yao ya kimsingi ya kununua na kuuza madini. “Kurejeshwa kwa minada Mirerani ni ushahidi wa nia ya Serikali ya kuhakikisha kuwa rasilimali za nchi zinasimamiwa kwa manufaa ya Watanzania wote, huu mfumo wa minada ni mzuri na elimu iendelee kutolewa kwa wingi ili watu waone manufaa na kujiingiza kwenye hii biashara” amesema Nkya. Awali, akizungumzia mfumo wa kidijitali unaotumika katika biashara hiyo Afisa Mwandamizi Biashara kutoka Soko la Bidhaa Tanzania (Tanzania Mercantile Exchange-TMX) Nicholaus Kaselwa amesema, Soko la Bidhaa Tanzania ni mfumo rasmi unaokutanisha wauzaji na wanunuzi kwa pamoja na kufanya biashara ya mkataba inayotoa uhakika wa ubora, ujazo na malipo hivyo ili kupata mafanikio makubwa inahitaji uwekezaji wa kisasa wa maghala. “Sisi tuna mfumo wa biashara ambako soko la bidhaa kama mnada huu hufanyika kwa kutumia mfumo wa kidijitali ambao huwawezesha wanunuzi wa bidhaa kufanya manunuzi popote walipo na kuweka bei zao za ushindani, mwenye bei nzuri hutangazwa mshindi na hupewa masaa 48 kulipia bidhaa na kuja kuchukua” ameongeza Kaselwa. Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Hafla ya Mnada wa Madini ya Vito Mirerani 2024 unaotarajiwa kufanyika Jumamosi hii Desemba 14, 2024

KURUDI KWA MINADA YA MADINI MIRERANI KUTASAIDIA KUONGEZA THAMANI YA MADINI – WADAU MADINI Read More »

Scroll to Top