TUME YA MADINI

CONTACT US | FAQs | STAFF MAIL | ENGLISH / SWAHILI

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF MINERALS

 THE MINING COMMISSION

mwanahamisi.msangi

WAZIRI MAVUNDE ATATUA MGOGORO WA MIPAKA YA LESENI MIRERANI.

▪️Awataka wachimbaji wote nchini kuzingatia sheria na kanuni za madini ▪️Alekeza Maafisa Madini kusimamia sheria ili kupunguza migogoro kwenye sekta ya Madini 📍Dodoma Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde amewataka wachimbaji kote nchini kuhakikisha wanazingatia sheria na kanuni ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima. Mh Mavunde ameyasema hayo jana Jijiji Dodoma wakati wa kikao cha kutatua mgogoro wa mipaka ya Leseni uliyopo kati ya Kampuni ya Njake na Ndg. Patrick Miroshi, ambapo alizikutanisha pande zote mbili zenye mgogoro huo na kujadili kwa pamoja namna ya kutatua mgogoro huo na mwishoni kufikia muafaka wa kila mmoja kuendelea na uchimbaji katika eneo la leseni yake kwa amani. “ Serikali inatamani kuona Sekta ya Madini inaendelea kukua na kutoa mchango wa ukuaji wa uchumi wa nchi yetu,migogoro siku zote inaturudisha nyuma katika jitihada za kuongeza uzalishaji na kuchochea Uchumi. Ni maelekezo ya Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan juu ya utatuzi wa haraka wa migogoro kwenye sekta ya madini ili kuchochea ukuaji wake. Niwatake maafisa Madini wote nchini kusimamia sheria na kanuni ili kupunguza migogoro isiyo ya lazima na pia niwatake wachimbaji wote kuzingatia sheria katika shughuli zao za kila siku”, alisema Mavunde. Baada ya Taarifa ya Timu ya wataalamu iliyoundwa na Waziri Mavunde ilielekezwa nankuridhiwa kuwa Pande mbili hizo kila mmoja kurejea kwenye eneo la mipaka ya Leseni yake na Kampuni ya Njake kumfidia Ndg. Miroshi gharama alizoingia awali za uchimbaji. Kikao hicho cha usuluhishi kilihudhuriwa na viongozi wa Wizara akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Mhandisi Yahya Samamba na Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwamo

WAZIRI MAVUNDE ATATUA MGOGORO WA MIPAKA YA LESENI MIRERANI. Read More »

INCREASED USE OF EXPLOSIVES IN TANZANIA SPARKS CALL FOR STRICTER REGULATIONS

Dodoma, January 13, 2025 The use of explosives in Tanzania has surged dramatically, rising from an average of 3,000 tons annually in the 1990s to 26,516.07 tons in 2024, a trend attributed to the expansion of mining, oil and gas exploration, and infrastructure projects. This was highlighted today by Engineer Ramadhani Lwamo, Acting Executive Secretary for the Mining Commission, during a session aimed at strengthening the capacity of mine and explosives inspectors in Dodoma. “The growing use of explosives underscores the increase in mining activities across the country. However, without proper oversight, this could result in catastrophic consequences,” Engineer Lwamo cautioned. He emphasized the urgent need for strict regulation to prevent accidents, noting, “This session is designed to empower inspectors to ensure miners’ safety and prevent injuries stemming from explosive misuse. Inspectors must take control of their regions to avoid tragedies that could tarnish the industry.” The session also revealed that Tanzania currently has over 231 magazines, 493 storage facilities, and 279 registered explosive storage boxes in use, underscoring the widespread nature of the explosives trade. Engineer Hamisi Kamando, Acting Mines Inspectorate and Environment Director, highlighted the dangers associated with non-compliance with existing laws, including the Explosives Act of 1963 and the Explosives Regulations of 1964. “Several accidents could have been prevented with proper adherence to the laws,” he said. In support, Senior Legal Officer Damian Kaseko urged inspectors to remain vigilant and adhere strictly to laws, policies, and regulations to avoid legal conflicts and ensure clarity in their roles. The growing demand for explosives has opened opportunities in Tanzania but has also introduced risks that necessitate robust oversight. As officials and stakeholders work to address these challenges, the focus remains on ensuring safety and minimizing harm in the burgeoning sector.

INCREASED USE OF EXPLOSIVES IN TANZANIA SPARKS CALL FOR STRICTER REGULATIONS Read More »

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA ITALIA KUENDELEZA SEKTA YA MADINI

▪️Mkutano wa Wafanyabiashara wa Tanzania na Italia kufanyika Mwezi Februari, 2025. ▪️Kampuni za Utengenezaji Vifaa kutoka vya Madini kutoka Italia kushiriki. ▪️Wachimbaji kunufaika na teknolojia na mitambo rafiki kwa mazingira 📍Dar es Salaam Waziri wa Madini, Mh. Anthony Mavunde (Mb) amesena kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na Italia katika kuendeleza sekta ya madini nchini hususani katika teknolojia na mitambo. Ameyasema hayo jana tarehe 06 Januari, 2025 alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mh. Giuseppe Coppola katika ofisi ndogo za Wizara ya Madini Jijini Dar es Salaam. “Rais wetu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameifungua nchi yetu kwa kuimarisha mahusiano kimataifa kupitia falsafa yake ya 4R. Sisi wasaidizi wake tutaendelea kuhakikisha tunasimamia maono hayo na kujenga mahusiano zaidi na washirika wetu kwa manufaa ya uchumi na wananchi wa pande zote. Zipo fursa nyingi kwenye sekta ya madini nchini kuanzia kwenye utafiti mpaka uongezaji thamani madini, mazingira ya uwekezaji ni mazuri hivyo ninawakaribisha sana wawekezaji kutoka nchini Italia kuja kuwekeza Tanzania“alisema Mavunde. Kwa upande wake Balozi Coppola, aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano inaompa tangu awasili nchini, na kusisitiza kwamba Italia inayo makampuni mengi ambayo yamejikita katika teknolojia hususan utengenezaji wa mitambo inayotumika kwenye sekta ya madini. “Mwezi Februari, 2025 tunataraji kuwa na mkutano wa wafanyabiashara baina ya Tanzania na Italia ambapo tunatarajia makampuni na wawekezaji katika sekta zote hususan madini kuja kushiriki mkutano huo. Ninaamini kwa kutumia mkutano huo utakuwa ni mwanzo mzuri wa wawekezaji kutoka Italia kuona fursa zilizopo nchini Tanzania na kuanza kuzichangamkia” alisisitiza Mhe. Coppola. Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde alionesha kufurahishwa na mpango wa mkutano wa wafanyabiashara wa Italia na Tanzania na kutanabaisha kwamba ni vizuri taarifa za kina kuhusu mkutano huo zikaifikia Wizara mapema kwa ajili ya uratibu ili wachimbaji wakubwa na wadogo waweze kushiriki kikamilifu na kuleta tija.

TANZANIA KUSHIRIKIANA NA ITALIA KUENDELEZA SEKTA YA MADINI Read More »

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI YA KUREJESHA HADHI YA MADINI YA TANZANITE

-Waziri Mavunde azindua mnada wa ndani Mirerani leo. – Minada ya ndani na nje ya nchi kutumika kutangaza madini ya vito. -Madini yote yatakayokosa wanunuzi kurejeshwa kwa wahusika -Wadau waonesha nia ya kujenga Mji wa Kimadini Mirerani Mirerani MANYARA: Waziri wa Madini Mheshimiwa Anthony Mavunde amesema Serikali imejidhatiti kurudisha hadhi ya Tanzanite kwa kufanya minada ndani na nje ya nchi ili kuyaongezea thamani na wafanyabiashara waweze kunufaika na kuongeza pato la taifa kwa ujumla. Waziri Mavunde ameyasema hayo leo Desemba 14, 2024 Mirerani mkoani Manyara wakati akizindua mnada wa madini ya vito ambao mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2017. Mheshimiwa Mavunde amesema mojawapo ya maeneo yanayosaidia kuongeza mapato ni pamoja na kudhibiti biashara ya madini, kuzuia utoroshaji na kuifanya biashara hiyo kuwa katika mfumo sahihi, uwepo wa minada utachochea uongezaji thamani ya madini ya vito. “Madini ya Vito yananunuliwa kwa asilimia kubwa kwa ajili ya ‘luxury’ ni ufahari na madini ya vito tunashindana na watu wengine ndio maana Serikali inaendelea kuchukua hatua, tunarudisha hadhi ya Tanzanite ili ikashindane vizuri duniani,”amesema Waziri Mheshimiwa Mavunde na kuongeza, “Moja ya hatua ya kwanza ni urejeshaji wa minada ya ndani na ya kimataifa, ili tuyape thamani madini yetu, duniani kuna madini mengi ya vito, moja ya sifa kubwa ya madini ya vito ni uadimu, Tanzanite ina sifa hizo; Ila sio madini pekee yake adimu, kuna nchi nyingine zina madini adimu ambayo hayapatikani popote hivyo tunashindana kimataifa ni lazima tuchukue hatua kuhakikisha tunarudisha hadhi ya Tanzanite katika soko la kimataifa ili na bei iweze kuongezeka na wafanyabiashara wanufaike,”amesisitiza Waziri Mavunde Amesema, katika vipengele (category) vya mawe duniani, jiwe linaanzia kuwa Precious, semi-Precious halafu baadaye linakuwa jiwe la kawaida na kwamba wanachukua hatua za makusudi ili Tanzanite lisiwe jiwe la kawaida. “Tukiacha liwe la kawaida mtanunua kwa kilo kwa gharama ndogo sana na mtashusha hadhi ya Tanzanite, Serikali haipo tayari kuona hilo linatokea ndio maana tunayafanya haya kwa ajili ya kuhakikisha tunalinda hadhi na heshima ya jiwe letu hili.” Amesisitiza Mheshimiwa Mavunde. Katika hatua nyingine, Waziri Mavunde amewahakikishia wadau wa madini kuwa Serikali haitachukua madini ya mtu baada ya mnada wa leo na kama kuna madini yatabaki yatakabidhiwa kwa wahusika. “Kumekuwepo na hisia na dhana baada ya mnada Serikali itachukua madini yaliyobaki kwa sababu katika mnada wa mwisho wa mwaka 2017 kuna madini yalibaki na wahusika hawakurejeshewa mpaka leo, nataka niwahakikishie Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kusimamia kuhakikisha katika biashara hii pia tuwajengee ‘confidence’ mtafanye biashara kwa uhuru na hakuna namna yoyote kuwa serikali itawaingilia na kuja kuyachukua madini yenu. “Yale madini yaliyochukuliwa yapo, yalibaki Benki Kuu ya Tanzania (BoT) tumeshayatoa na tutawakabidhi rasmi wahusika ili waendelee na biashara yao ya madini, nataka niwatoe hofu na muwe na amani,”amesema Waziri Mavunde. “Manyara tayari mna eneo ambalo tutajenga ‘Tanzanite Exchange Centre’ ambayo kwa sasa tumefanya mazungumzo na wadau tutajenga kitu kinaitwa ‘Tanzanite Smart City’ ambao utakuwa mji mkubwa wenye hoteli ndani yake, Helikopta ambazo zitatua humo humo, ukumbi mkubwa wa mikutano wahusika hivi sasa wapo Wizara ya fedha, likikamilika hili natamani siku moja mkutano mkubwa wa madini ufanyike Mirerani.”Amesema. Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo ameongeza kuwa kupitia mnada huu uliozinduliwa leo, idadi ya wauzaji waliojisajili kwenye mfumo wa kielektroniki wa kuendesha minada ni 195 wakiwemo wafanyabiashara wadogo wa madini (brokers) 120, wafanyabiashara wakubwa wa madini (dealers) 59, waongeza thamani madini (lapidary) 7 na wachimbaji madini 9. Kiasi cha madini kilicholetwa kwenye mnada ni kilogramu 184.06 kinachokadiriwa kuwa na thamani ya shilingi za kitanzania bilioni 3.10. Wakati huohuo akizungumza kwenye uzinduzi wa mnada huo Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda amempongeza Waziri wa Madini kwa kuweka nguvu kubwa kwenye utafiti wa madini kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) na kuwezesha wachimbaji kuchimba bila kupoteza mitaji ikiwa ni sehemu ya “Vision 2030 ya Madini ni Maisha na Utajiri,” na kuongeza kuwa, “Kamati itaendelea kutoa ushirikiano kwa Wizara lengo likiwa ni kuhakikisha mchango wa Sekta ya Madini unakua na kufikia asilimia 10 ifikapo mwaka 2025” Naye Mbunge wa Simanjiro Mheshimiwa Christopher Ole Sendeka amepongeza jitihada za Serikali kwa kupania kuleta mapinduzi ya kiuchumi ikiwa ni pamoja na uanzishwaji wa masoko na vituo vya ununuzi wa madini nchini, kuhakikisha dhahabu inanunuliwa kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) hivyo kuendelea kuimarisha uchumi wa nchi. “Ninashauri Serikali kuendelea kutilia mkazo wa biashara ya madini ya vito kuendelea kufanyika katika mji wa Mirerani wakati ujenzi wa Soko la Madini Mirerani ukiendelea” amesisitiza. Naye Mkuu wa Mkoa wa Manyara , Mheshimiwa Queen Sendiga ameongeza kuwa minada ya madini ya vito italeta manufaa makubwa kwa nchi ikiwa ni pamoja na kukuza kipato kwa wachimbaji na wafanyabiashara wa madini, serikali kupata mapato, kuimarisha ubora wa madini ya vito na kuongeza ushiriki wa watanzania katika Sekta ya Madini na kuwataka wananchi kuchangamkia fursa za uwekezaji katika Sekta ya Madini.

SERIKALI YABAINISHA MIKAKATI YA KUREJESHA HADHI YA MADINI YA TANZANITE Read More »

KURUDI KWA MINADA YA MADINI MIRERANI KUTASAIDIA KUONGEZA THAMANI YA MADINI – WADAU MADINI

  🔹️ Biashara kufanyika kidijitali kupitia Soko la Bidhaa Tanzania-TMX 🔹️ Waziri Mavunde kuwa Mgeni Rasmi Hafla ya Mnada 🔹️ Wanawake wahamasishwa kuchangamkia fursa za biashara katika mnyororo wa madini_ 📍 Mirerani- Manyara Wafanyabiashara wa Madini nchini Tanzania wameelezea matumaini yao makubwa kuhusu hatua ya kurejeshwa kwa Minada ya Madini katika eneo Mirerani, Mkoa wa Manyara na kueleza kuwa kurejea kwa minada hiyo kutasaidia kuleta mchango mkubwa katika kuongeza thamani ya madini, hususan Tanzanite, ambayo ni madini adimu yanayopatikana nchini Tanzania pekee. Hayo yameelezwa kwa nyakati tofauti na baadhi ya wafanyabiashara wakati wakizungumza na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Madini leo Desemba 13, 2024 kuelekea Siku ya Mnada wa Madini ya Vito Mirerani 2024 inayotarajiwa kufanyika Desemba 14, 2024. Wafanyabiashara hao wameitaka Serikali kuendelea kushirikiana na wadau ili kuhakikisha kuwa minada inafanyika mara kwa mara, kwa uwazi, na kwa misingi ya haki, ili kutoa faida kwa pande zote zinazohusika. Kwa pamoja, wanatarajia kuwa kurudi kwa minada ya madini Mirerani kutakuwa ni hatua muhimu ya kuimarisha thamani ya madini ya Tanzania na kukuza uchumi wa taifa. Akizungumzia Mnada huo, Mfanyabiashara wa Madini (Dealer) Upendo Kibona ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Lucid Dream Limited amesema kuwa kurejea kwa minada ya madini Mirerani itaongeza uwazi katika soko la madini na kuhakikisha kuwa wauzaji wanapata bei stahiki kutokana na ushindani wa moja kwa moja kati ya wanunuzi. “Kwa kweli tunaishukuru sana Serikali kwa kurejesha minada hii, kwasababu inatupa fursa ya kuuza madini yetu kwa bei ya ushindani, pamoja na kuwa huu ni mnada wa ndani lakini utasaidia kuongeza ushindani katika bei, na hata hiyo minada ya kimataifa itakapoanza nadhani tutakuwa sehemu nzuri zaidi” amesema Kibona. Kwa upande wake, Broker wa Madini Glory Robinson amesema, matarajio yake ni kuona minada hiyo inachochea uchumi wa ndani kupitia ajira na biashara ndogo ndogo zinazotegemea shughuli za madini na kwamba Mirerani inaweza kuwa kitovu cha maendeleo ya kiuchumi kwa Mkoa wa Manyara, kwa kuwa minada huvutia wanunuzi wa ndani na nje ya nchi, ambao pia hutumia huduma za hoteli, usafiri, na bidhaa nyingine za ndani. “Niwahamasishe wanawake wenzangu kuchangamkia hii fursa, kwa sababu kupitia biashara zilizopo kwenye mnyororo mzima wa shughuli za madini zinaweza kuwasaidia kuinua vipato vyao na kuendesha maisha yao sambamba na kutunza Familia zao” amesisitiza Glory. Naye, Broker wa Madini Sweety Nkya, amesema kuwa Serikali imeonyesha dhamira ya kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mkubwa zaidi kwa pato la taifa ambako kupitia mifumo hiyo ya Minada, biashara itafanyika kwa haki na washindi watapata haki yao ya kimsingi ya kununua na kuuza madini. “Kurejeshwa kwa minada Mirerani ni ushahidi wa nia ya Serikali ya kuhakikisha kuwa rasilimali za nchi zinasimamiwa kwa manufaa ya Watanzania wote, huu mfumo wa minada ni mzuri na elimu iendelee kutolewa kwa wingi ili watu waone manufaa na kujiingiza kwenye hii biashara” amesema Nkya. Awali, akizungumzia mfumo wa kidijitali unaotumika katika biashara hiyo Afisa Mwandamizi Biashara kutoka Soko la Bidhaa Tanzania (Tanzania Mercantile Exchange-TMX) Nicholaus Kaselwa amesema, Soko la Bidhaa Tanzania ni mfumo rasmi unaokutanisha wauzaji na wanunuzi kwa pamoja na kufanya biashara ya mkataba inayotoa uhakika wa ubora, ujazo na malipo hivyo ili kupata mafanikio makubwa inahitaji uwekezaji wa kisasa wa maghala. “Sisi tuna mfumo wa biashara ambako soko la bidhaa kama mnada huu hufanyika kwa kutumia mfumo wa kidijitali ambao huwawezesha wanunuzi wa bidhaa kufanya manunuzi popote walipo na kuweka bei zao za ushindani, mwenye bei nzuri hutangazwa mshindi na hupewa masaa 48 kulipia bidhaa na kuja kuchukua” ameongeza Kaselwa. Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Hafla ya Mnada wa Madini ya Vito Mirerani 2024 unaotarajiwa kufanyika Jumamosi hii Desemba 14, 2024 Mirerani Mkoani Manyara.

KURUDI KWA MINADA YA MADINI MIRERANI KUTASAIDIA KUONGEZA THAMANI YA MADINI – WADAU MADINI Read More »

COMPREHENSIVE STRATEGIES SET TO BOOST THE MINERAL SECTOR

  Dodoma Today, December 5, 2024, the first meeting of the new Commision for the Mining Commission was held in Dodoma, following the appointment of the new Chairperson of the Mining Commission, Janet Reuben Lekashingo. The meeting brought together Commissioners of the Commission and the Management Team to receive and discuss the quarterly implementation report of the Commission’s duties. Speaking at the meeting, the Chairperson, Janet Lekashingo, commended the Mining Commission for its excellent work, particularly in revenue collection, managing mineral markets and buying centers established in the country, enhancing safety in mining activities, local content and corporate social responsibility During the meeting, various strategies were outlined through the Technical, Human Resources, Financial, and Local Content Committees to further develop the sector.

COMPREHENSIVE STRATEGIES SET TO BOOST THE MINERAL SECTOR Read More »

NAIBU SPIKA MGENI ASISITIZA UJENZI WA VIWANDA VYA UONGEZAJI THAMANI MADINI NCHINI

*_Aishukuru GST kwa kufanya utafiti wa madini na kuandaa Ramani ya Jiolojia Zanzibar_* *_Awakaribisha Wawekezaji Kuwekeza Katika Sekta ya Madini Zanzibar_* *_Waziri Mavunde asema Wizara itaandaa eneo maalum la kudumu la kufanyia Mikutano ya Madini_* Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mgeni Hassan Juma, amesema kuwa kama ili kufikia azma ya kuwa kitovu cha madini barani Afrika ni lazima kujenga viwanda vitakavyoongeza thamani ya malighafi na kuzalisha bidhaa za mwisho tayari kwa soko la ndani na nje ikiwemo masoko makubwa duniani. Amesema hayo, leo Novemba 21, 2024, wakati akifunga Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini 2024 uliofanyika kwa siku tatu (Novemba 19-21, 2024) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, Mhe. Mgeni ameeleza kuwa mijadala iliyofanyika kupitia Mkutano huo imejikita katika kutafuta suluhisho la changamoto zinazoikabili Sekta ya Madini, hususan katika nyanja za mitaji na teknolojia ya kisasa katika uongezaji thamani madini na kwamba kupitia maazimio yaliyotolewa na washiriki, Serikali imepata mapendekezo yatakayofanyiwa kazi kwa manufaa ya sekta na taifa kwa ujumla. “Uongezaji thamani madini ni jambo la msingi kwa maendeleo yetu. Tunapaswa kujenga viwanda vitakavyoongeza thamani ya malighafi na kuzalisha bidhaa za mwisho tayari kwa soko la ndani na nje,” amesema Mhe. Mgeni. Aidha, amesisitiza kuwa, Mkutano huo, uliobebwa na Kaulimbiu ya “Uongezaji Thamani Madini kwa Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii”, umekuwa jukwaa muhimu kwa kubadilishana uzoefu, kukuza mitandao na wadau, na kuibua majadiliano ya kitaalamu kuhusu mustakabali wa sekta ya madini nchini hususan katika eneo la uongezaji thamani madini. Mhe. Mgeni ameongeza kuwa, Kampuni mbalimbali zinazoshughulika na mnyororo wa thamani wa madini zimepata nafasi ya kushiriki mkutano huo, na kwamba matumaini yake ni kuwa zimejifunza kwa kina kuhusu Sera za Madini za Tanzania hivyo zitaendelea kuchangamkia fursa zilizopo ndani ya sekta ya madini hapa nchini. Katika hatua nyingine, Mhe. Mgeni ameipongeza na kuishukuru Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kwa juhudi zake za kufanya utafiti wa madini visiwani Zanzibar na kisha kuandaa ramani ya jiolojia ya visiwa hivyo. Mhe. Mgeni amesema kuwa kupitia Ripoti ya Utafiti wa Madini Visiwani Zanzibar iliyokabidhiwa na GST hivi karibuni visiwani humo, imesaidia kujua utajiri mkubwa wa rasilimali madini uliopo visiwani humo na kwamba Zanzibar iko tayari kuendeleza rasilimali madini yaliyoanishwa kwa mujibu wa Sheria. “Kipekee tunaishukuru sana GST kwa hatua kubwa ya kutufanyia utafiti wa Visiwa vyetu. Nitumie fursa hii kuwakaribisha wawekezaji wote waliowekeza katika Sekta ya Madini hapa bara kufikiria kuwekeza pia Zanzibar kwa lengo la kuyaendeleza madini yetu.” Amesema Mhe. Mgeni. Kwa upande wake, Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amesisitiza kuwa, Mkutano huo umekuwa na mafanikio makubwa, kwani kwa mwaka 2024 umeleta washiriki zaidi ya 1500 kutoka Afrika na nje ya Africa kwa nia ya kubadilishana uzoefu. “Kutokana na mahudhurio makubwa ya washiriki, tunafikiria kuwa na eneo letu maalum kwa ajili ya Mikutano ya Sekta ya Madini kama ilivyo kwa Mining Indaba kule Afrika Kusini, na ninawaomba Wakuu wa Mikoa kutenga maeneo maalum katika mikoa yao kwa ajili ya mikutano hii ya madini” amesema Mavunde. Akizungumzia Kuhusu Sekta ya Madini visiwani Zanzibar, Mhe. Mavunde amesema “Watu wakisikia Zanzibar wanachofikiria ni utalii, lakini miezi michache iliyopita Ripoti ya Utafiti wa Madini kule Zanzibar, Pemba yamegundulika madini tembo (Heavy Mineral Sands) hivyo kupitia rasilimali hiyo tunaamini uwekezaji mkubwa utafika pemba na tutaona manufaa ya uwepo wa rasilimali hizo na itasaidia kufungua uchumi wa Zanzibar“ Naye, Waziri wa Maji, Nishati na Madini Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Shaib Hassan Kaduara amesema kuwa, kama taifa moja ni muhimu kuimarisha ushirikiano katika eneo la utafiti wa kina wa madini kwa manufaa ya pande zote na kuongeza kuwa “Ni fahari kubwa kujua tuna rasilimali hizi na tunaahidi kuzisimamia kwa manufaa ya vizazi vilivyopo na vijavyo” Awali akizungumza Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amesema kuwa, Kaulimbiu ya Mkutano “Uongezaji Madini Thamani kwa Maendeleo ya Kiuchumi kwa Jamii” (Mineral Value Addition for Social – Economic Development) ikiwa na lengo la kuhamasisha shughuli za uongezaji thamani madini nchini kwa maendeleo ya Kiuchumi kwa Jamii. Aidha, Dkt. Kiruswa amebaisha kuwa, Kaulimbiu hiyo inaenda sambamba na utekelezaji wa Sera ya Madini ya 2009 ambayo inaitaka Serikali kuhakikisha madini yanayozalishwa nchini yanaongezewa thamani kabla ya kusafirishwa kwenda nje ya nchi ili kupanua wigo wa mnyororo wa thamani kupitia fursa za ajira na uanzishwaji wa viwanda vya kuchakata madini nchini. Mkutano wa mwaka huo wa Uwekezaji wa Katika Sekta ya Madini 2024 umedhihirisha nafasi ya Tanzania kama kitovu cha uwekezaji katika sekta ya madini, na umefungua njia kwa Zanzibar kushiriki kwa kina katika mpango wa maendeleo endelevu ya rasilimali madini.

NAIBU SPIKA MGENI ASISITIZA UJENZI WA VIWANDA VYA UONGEZAJI THAMANI MADINI NCHINI Read More »

ALIYOYASEMA NAIBU WAZIRI WA MADINI, DKT. STEVEN KIRUSWA KATIKA KIPINDI CHA JAMBO TANZANIA

Royal Tour imeleta wawekezaji Royal tour imeongeza mwamko wa wawekezaji kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Madini Tanzania. Madini tunayo na wawekezaji wameendelea kuja. Kuna ongezeko la wazalishaji, Wadogo, wa Kati na Wakubwa. Ujenzi wa Kiwanda cha Kusafisha Madini ya Metali Mwekezaji wa sasa Kampuni ya Tembo Nickel Refining Limited itakayojenga kiwanda cha kusafisha madini ya metali hivi sasa yupo kwenye mchakato wa kujenga Kiwanda cha kisasa cha kusafisha madini hayo, katika eneo la Mgodi wa unaofungwa wa Buzwagi pale Kahama mkoani Shinyanga. Mkakati wa Tanzania kuongeza thamani Nchini Mkakati wa kuyaongezea thamani madini hapa nchini upo bayana. Tunataka kama taifa kuhakikisha taifa linajengewa uwezo wa kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanda vya kuchakata madini mkakati hapa hapa nchini hatua hii itasaidia kulinda ajira za watanzania. Minada ya Madini ya ndani na nje ya Nchi Mbioni Katika mwelekeo wa kuendelea kutangaza madini yetu na kuongeza masoko tutaanzisha minada ya madini ya vito ya ndani na ya kimataifa, minada ya ndani inatarajiwa kufanyika katika miji ya Arusha, Dar Es Salaam na Zanzibar. Utoroshaji Madini Kukosekana kwa masoko ya madini kulichangia utoroshaji wa madini kwasababu hakukuwa na mfumo rasmi lakini pia baadhi walikosa uzalendo. Tunaendelea kuzunguka nchi nzima kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kutumia masoko. Kwa kushirikiana na Vyombo vya dola tumeendelea kudhibiti utotoshaji wa madini hadi katika viwanja vya ndege. Tumeanzisha masoko 43 na vituo vya ununuzi 105 kwa ajili ya kudhibiti utoroshaji wa madini na hatimaye kulinda mapato ya Serikali. Mazingira Wezeshi shughuli za Madini Serikali imeendelea kupeleka huduma mbalimbali kwenye shughuli za madini ikiwemo miundombinu ya barabara, umeme kuhakikisha shughuli za madini zinafanyika vizuri kuongeza tija. Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR) Tumeweka Sheria na Kanuni zinzomtakamwekezaji kuwajibika kwa jamii inayomzunguka Ili wanufaike na uwekezaji wao. Kwanza hapatuna dhana mbili, moja kuwajibikakwa jamii, pili inamtaka atoe ajira kwa watanzania wanaozunguka maeneo ya uwekezaji kupitia utoaji huduma migodini. Maudhui ya Ndani (Local Content) Tumefanikiwa kutengeneza Sheria na Kanuni zinazowataka wamiliki wa migodi kununua bidhaa na huduma ambazo zinapatikana hapa nchini basi wanunulie hapa na kutoka kwa watanzania, kufanya hivyo kutoka kwa Kampuni za Watanzania, na tangu ianze kutekelezwa imeleta mabadiliko makubwa sana katika sekta ya madini na wananchi waliopo katika maeneo shughuli za madini zinapofanyika ni mashahidi katika hili. Mazingira Kabla ya mwekezaji kufanya shughuli za uchimbaji ni lazima aandae taarifa ya athari za mazingira namna ya kurejesha katika hali yake ya asili baada ya uchimbaji. Madini kama Uranium tathmini yake inafanyika kwa mapana zaidi, Sisi wizarani tuna vitengo vyote vinavyosimamia masuala ya afya, usalama na utunzaji mazingira kikiwemo cha ukaguzi wa migodi. Matumizi wa Zebaki Tanzania inachukua hatua kila siku kwa kuhamasisha matumizi yateknolojia rahisi na kuachana na matumizi ya zebaki tunapoelekea katika kipindi cha ukomo wa matumizi haya. Tuna Jambo Letu Dar Es Salaam Novemba 19- 21, 2024 Kila mwaka tunakutana katika Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini, Ni mkutano unaotumika kutangaza fursa zetu za uwekezaji kwenye Sekta ya Madini ikihusisha watoa mada kutoka ndani na nje. Ninawahamasisha wadau mbalimbali kujisajili ili kushiriki Mkutano huo muhimu.

ALIYOYASEMA NAIBU WAZIRI WA MADINI, DKT. STEVEN KIRUSWA KATIKA KIPINDI CHA JAMBO TANZANIA Read More »

ALIYOYAZUNGUMZA WAZIRI WA MADINI KATIKA KIPINDI CHA GOOD MORNING CHA WASAFI TV NA RADIO

Makusanyo na Mafanikio ya Sekta ya Madini Mwaka wa Fedha 2015/16: Sekta ya Madini ilikusanya shilingi bilioni 161. Mwaka wa Fedha 2023/24: Makusanyo yaliongezeka hadi bilioni 753. Mwaka wa Fedha 2024/25: Lengo la makusanyo ni trilioni 1, ambapo katika robo ya kwanza pekee zimepatikana zaidi ya milioni 300. Mafanikio haya yanatokana na Mabadiliko ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017, ambayo yameimarisha ufuatiliaji na uwazi katika sekta. Uanzishwaji wa Masoko na Vituo vya Ununuzi Masoko 43 na vituo vya ununuzi 105 vimeanzishwa kudhibiti utoroshaji wa madini na kuongeza uwazi katika biashara. Hatua hiyo imesaidia kudhibiti utoroshaji wa madini lakini kwa wale wachache waliokamatwa wakitorosha madini na kupatikana na mahakama kuwakuta na hatia, Serikali imechukua hatua kali ikiwemo kufuta leseni zao na hawaruhusiwi kufanya biashara ya madini tena hapa nchini. Mazingira Bora kwa Wachimbaji Wadogo Mmnamo mwaka 2019: Wachimbaji walikuwa wakilipa zaidi ya asilimia 30.3 ya mapato yao kama kodi na tozo lakini baada ya Serikali kusikiliza changamoto zao, hivisasa, Serikali imepunguza tozo na kodi hadi asilimia 9.3, na wachimbaji wanaopeleka dhahabu kwenye mitambo ya kusafisha hawalipi mrabaha, hivyo wanabakiwa na asilimia 4 tu. Serikali imekuwa ikiwekeza kwa kuwasaidia wachimbaji wadogo, ikiwemo manunuzi ya mitambo ya uchorongaji kupitia STAMICO ili kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza tija. Pia, Serikali kupitia Wizara ya Madini imeanzisha program maalum ya Mining for Brighter Tomorrow (MBT) kwa lengo kusaidia vijana na wanawake kujihusisha katika uchimbaji wenye manufaa. Kuhusu Madini ya Almasi na Tanzanite Almasi: Mahitaji duniani yameshuka kutokana na ongezeko la almasi za maabara. Tanzanite: Serikali imerejesha hadhi ya madini haya kwa kutunga sheria na kurudisha masoko ya ndani. Sheria mpya inaruhusu minada ya ndani na ya kimataifa ya madini ya vito. Maudhui ya Ndani (local Content) na Ajira kwa Wazawa Ajira za moja kwa moja kwa Watanzania katika sekta ya madini zimefikia zaidi ya 16,000, huku nafasi za juu kwa baadi ya miradi mikubwa zikiwa mikononi mwa watanzania wazawa. Kampuni za Kitanzania zinashiriki moja kwa moja katika kusambaza bidhaa na huduma kwa migodi Mikubwa hali inayopelekea kunongeza ajira kwa Watanzania na mzunguko wa fedha kubaki hapa nchini.   Madini Mkakati na Muhimu kwa Teknolojia ya Kisasa Tanzania ina madini muhimu yanayotumika katika teknolojia za hali ya juu na viwanda: Kinywe (Graphite): Muhimu katika utengenezaji wa betri, hasa kwa magari ya umeme. Nikeli: Hutumika katika chuma kisichoshika kutu na betri za lithiamu-ioni. Kobalti: Hutumika kwa betri na uhifadhi wa nishati. Lithiamu: Muhimu kwa betri za magari ya umeme. Madini Adimu ya Ardhi (Rare Earth Elements REEs): Kama niobium na tantalum, yanayotumika katika simu, mitambo ya upepo, na vifaa vya kijeshi. Mkakati wa Kuongezea Thamani Madini Nchini Malengo ya 2050: Dunia inapanga kuachana na magari ya petrol na dizeli. Tanzania imejikita katika kuongeza thamani ya madini hapa nchini badala ya kuyasafirisha ghafi, ili kuboresha ajira na uchumi. Kiwanda cha Kusafisha Makinikia: Hekari zaidi ya 1300 zimetengwa Buzwagi kwa ajili ya kiwanda cha kusafisha madini, ambako Nikeli kutoka Kabanga Nickel itasafishwa. Leseni ya uchimbaji haitatolewa kwa wawekezaji ambao hawajawasilisha mpango wa kujenga kiwanda cha kusafisha madini hapa nchini, kwa mujibu wa sheria ili kulinda ajira za watanzania. Gesi ya Helium na Fursa kwa Madini ya Kinywe Tanzania ina hifadhi kubwa ya gesi ya Helium katika Songwe na Rukwa, inayotumika katika vifaa vya matibabu kama MRI. Tanzania ni ya tatu Afrika kwa uzalishaji wa Kinywe (Graphite), na mradi mkubwa unatarajiwa kuongeza uzalishaji ili kuimarisha nafasi ya nchi katika sekta hii duniani kote.Kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini 2024 Tarehe: Novemba 19-21, 2024. Mahali: Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam. Mkutano huu unaleta pamoja wawekezaji, viongozi na wawaziri wa kisekta kutoka nchi mbalimbali, na maafisa kutoka nchi mbalimbali kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kukuza uwekezaji katika sekta ya madini. Kipekee, tunamshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini, mfano kampuni ya BHP inatarajiwa kurudi kuwekeza nchini kupitia mradi wa Kabanga Nickel baada ya kusitisha shughuli zake barani Afrika zaidi ya miaka 15 iliyopita.    

ALIYOYAZUNGUMZA WAZIRI WA MADINI KATIKA KIPINDI CHA GOOD MORNING CHA WASAFI TV NA RADIO Read More »

LEKASHINGO ATAKA USHIRIKIANO TUME YA MADINI

• Ampa Tano Rais Samia • Ahaidi kuipaishaa Tume MWENYEKITI Mpya wa Tume ya Madini, Janet Lekashingo ameahidi kufanya kazi kwa uadilifu, uaminifu na ushirikiano mkubwa na watumishi na wadau wote wa Sekta ya Madini. Lekashingo ametoa ahadi hiyo leo Novemba 8, 2024 akiripoti ofisi za Tume ya Madini zilizopo Kikuyu, jijini Dodoma tayari kuanza majukumu yake mapya baada ya kuteuliwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan Oktoba 31, 2024 kuwa Mwenyekiti mpya wa Kamisheni ya Tume ya Madini akichukua nafasi ya Profesa Indris Kikula ambaye muda wake umemalizika. Amesema, Sekta ya Madini ina nafasi kubwa ya kubadili mtazamo wa nchi, kubadili maisha ya watanzania pia kubadili uchumi wa nchi. “Hivyo ni muhimu sisi watumishi wa Tume ya Madini kuhakikisha kwamba tunaangalia mifumo yetu kama inastahili, kuhakikisha mazingira maeneo ya migodini yanatuzwa, kuhakikisha jamii inashirikishwa, nimefurahi kusikia wachimbaji wadogo wanapewa umuhimu unaostahili,”amesema Lekashingo. Aidha, amesema amefarijika kurudi Tume ya Madini kama Mwenyekiti wa Kamisheni na kumshukuru Rais Dkt. Samia kwa kumuamini na kumpa jukumu hilo muhimu la kuongoza Tume ya Madini. “Pia nimshukuru Mheshimiwa Waziri wa Madini Anthony Mavunde, Katibu Mkuu Mhandisi Yahya Samamba na viongozi wote kwa kuwa nami katika safari hii,”amesema Lekashingo na kuongeza “Wengi mnafahamu nimepata bahati ya kutumika kama Kamishna wa Tume ya Madini na ninaelewa madini yana umuhimu mkubwa katika uchumi wetu hivyo ni jukumu letu kupitia Tume kuhakikisha Wizara inafanya vizuri kutunza mazingira na madini yananufaisha watanzania na uchumi wa nchi yetu,”amesisitiza. Awali, akitoa taarifa ya Tume ya Madini Kaimu Mkurugenzi wa Leseni na Tehama, Mhandisi Aziza Swedi kwa niaba ya Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini Mhandisi Ramadhani Lwamo, amesema Tume ya Madini imeendelea kuimarisha ukusanyaji wa maduhuli yatokanayo na madini ambapo kiwango cha makusanyo ya maduhuli ya Serikali kilipanda kutoka Shilingi Bilioni 346.275 zilizokusanywa Mwaka 2018/2019 na kufikia Shilingi Bilioni 753.18 Mwaka 2023/2024. Aidha, amesema katika Mwaka wa Fedha 2024/2025, Tume ya Madini imepangiwa kukusanya jumla ya Shilingi Bilioni 999. 998, ambapo hadi kufikia Oktoba 31, 2024 Tume imefanikiwa kukusanya jumla ya Shilingi Bilioni 354. 613 sawa na asilimia 35.46 ya lengo la mwaka. Makusanyo ya mwezi Oktoba ni Shilingi Bilioni 96.724 sawa na asilimia 116.07 ya lengo la mwezi Oktoba 2024. Mhandisi Swedi amesema, mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa umeimarika na kufikia asilimia 9.0 Mwaka 2023 ikilinganishwa na asilimia 5.1 kwa mwaka 2018. Aidha, ukuaji wa Sekta ya Madini uliimarika na kufikia asilimia 11.3 kwa Mwaka 2023 ikilinganishwa na asilimia 5.1 Mwaka 2018.  

LEKASHINGO ATAKA USHIRIKIANO TUME YA MADINI Read More »

Scroll to Top