TUME YA MADINI

CONTACT US | FAQs | STAFF MAIL | ENGLISH / SWAHILI

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

MINISTRY OF MINERALS

 THE MINING COMMISSION

Announcements

ALIYOYASEMA NAIBU WAZIRI WA MADINI, DKT. STEVEN KIRUSWA KATIKA KIPINDI CHA JAMBO TANZANIA

Royal Tour imeleta wawekezaji Royal tour imeongeza mwamko wa wawekezaji kuja kuwekeza kwenye Sekta ya Madini Tanzania. Madini tunayo na wawekezaji wameendelea kuja. Kuna ongezeko la wazalishaji, Wadogo, wa Kati na Wakubwa. Ujenzi wa Kiwanda cha Kusafisha Madini ya Metali Mwekezaji wa sasa Kampuni ya Tembo Nickel Refining Limited itakayojenga kiwanda cha kusafisha madini ya metali hivi sasa yupo kwenye mchakato wa kujenga Kiwanda cha kisasa cha kusafisha madini hayo, katika eneo la Mgodi wa unaofungwa wa Buzwagi pale Kahama mkoani Shinyanga. Mkakati wa Tanzania kuongeza thamani Nchini Mkakati wa kuyaongezea thamani madini hapa nchini upo bayana. Tunataka kama taifa kuhakikisha taifa linajengewa uwezo wa kuwekeza kwenye ujenzi wa viwanda vya kuchakata madini mkakati hapa hapa nchini hatua hii itasaidia kulinda ajira za watanzania. Minada ya Madini ya ndani na nje ya Nchi Mbioni Katika mwelekeo wa kuendelea kutangaza madini yetu na kuongeza masoko tutaanzisha minada ya madini ya vito ya ndani na ya kimataifa, minada ya ndani inatarajiwa kufanyika katika miji ya Arusha, Dar Es Salaam na Zanzibar. Utoroshaji Madini Kukosekana kwa masoko ya madini kulichangia utoroshaji wa madini kwasababu hakukuwa na mfumo rasmi lakini pia baadhi walikosa uzalendo. Tunaendelea kuzunguka nchi nzima kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kutumia masoko. Kwa kushirikiana na Vyombo vya dola tumeendelea kudhibiti utotoshaji wa madini hadi katika viwanja vya ndege. Tumeanzisha masoko 43 na vituo vya ununuzi 105 kwa ajili ya kudhibiti utoroshaji wa madini na hatimaye kulinda mapato ya Serikali. Mazingira Wezeshi shughuli za Madini Serikali imeendelea kupeleka huduma mbalimbali kwenye shughuli za madini ikiwemo miundombinu ya barabara, umeme kuhakikisha shughuli za madini zinafanyika vizuri kuongeza tija. Uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii (CSR) Tumeweka Sheria na Kanuni zinzomtakamwekezaji kuwajibika kwa jamii inayomzunguka Ili wanufaike na uwekezaji wao. Kwanza hapatuna dhana mbili, moja kuwajibikakwa jamii, pili inamtaka atoe ajira kwa watanzania wanaozunguka maeneo ya uwekezaji kupitia utoaji huduma migodini. Maudhui ya Ndani (Local Content) Tumefanikiwa kutengeneza Sheria na Kanuni zinazowataka wamiliki wa migodi kununua bidhaa na huduma ambazo zinapatikana hapa nchini basi wanunulie hapa na kutoka kwa watanzania, kufanya hivyo kutoka kwa Kampuni za Watanzania, na tangu ianze kutekelezwa imeleta mabadiliko makubwa sana katika sekta ya madini na wananchi waliopo katika maeneo shughuli za madini zinapofanyika ni mashahidi katika hili. Mazingira Kabla ya mwekezaji kufanya shughuli za uchimbaji ni lazima aandae taarifa ya athari za mazingira namna ya kurejesha katika hali yake ya asili baada ya uchimbaji. Madini kama Uranium tathmini yake inafanyika kwa mapana zaidi, Sisi wizarani tuna vitengo vyote vinavyosimamia masuala ya afya, usalama na utunzaji mazingira kikiwemo cha ukaguzi wa migodi. Matumizi wa Zebaki Tanzania inachukua hatua kila siku kwa kuhamasisha matumizi yateknolojia rahisi na kuachana na matumizi ya zebaki tunapoelekea katika kipindi cha ukomo wa matumizi haya. Tuna Jambo Letu Dar Es Salaam Novemba 19- 21, 2024 Kila mwaka tunakutana katika Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji katika Sekta ya Madini, Ni mkutano unaotumika kutangaza fursa zetu za uwekezaji kwenye Sekta ya Madini ikihusisha watoa mada kutoka ndani na nje. Ninawahamasisha wadau mbalimbali kujisajili ili kushiriki Mkutano huo muhimu.

ALIYOYASEMA NAIBU WAZIRI WA MADINI, DKT. STEVEN KIRUSWA KATIKA KIPINDI CHA JAMBO TANZANIA Read More »

ALIYOYAZUNGUMZA WAZIRI WA MADINI KATIKA KIPINDI CHA GOOD MORNING CHA WASAFI TV NA RADIO

Makusanyo na Mafanikio ya Sekta ya Madini Mwaka wa Fedha 2015/16: Sekta ya Madini ilikusanya shilingi bilioni 161. Mwaka wa Fedha 2023/24: Makusanyo yaliongezeka hadi bilioni 753. Mwaka wa Fedha 2024/25: Lengo la makusanyo ni trilioni 1, ambapo katika robo ya kwanza pekee zimepatikana zaidi ya milioni 300. Mafanikio haya yanatokana na Mabadiliko ya Sheria ya Madini ya mwaka 2017, ambayo yameimarisha ufuatiliaji na uwazi katika sekta. Uanzishwaji wa Masoko na Vituo vya Ununuzi Masoko 43 na vituo vya ununuzi 105 vimeanzishwa kudhibiti utoroshaji wa madini na kuongeza uwazi katika biashara. Hatua hiyo imesaidia kudhibiti utoroshaji wa madini lakini kwa wale wachache waliokamatwa wakitorosha madini na kupatikana na mahakama kuwakuta na hatia, Serikali imechukua hatua kali ikiwemo kufuta leseni zao na hawaruhusiwi kufanya biashara ya madini tena hapa nchini. Mazingira Bora kwa Wachimbaji Wadogo Mmnamo mwaka 2019: Wachimbaji walikuwa wakilipa zaidi ya asilimia 30.3 ya mapato yao kama kodi na tozo lakini baada ya Serikali kusikiliza changamoto zao, hivisasa, Serikali imepunguza tozo na kodi hadi asilimia 9.3, na wachimbaji wanaopeleka dhahabu kwenye mitambo ya kusafisha hawalipi mrabaha, hivyo wanabakiwa na asilimia 4 tu. Serikali imekuwa ikiwekeza kwa kuwasaidia wachimbaji wadogo, ikiwemo manunuzi ya mitambo ya uchorongaji kupitia STAMICO ili kupunguza gharama za uzalishaji na kuongeza tija. Pia, Serikali kupitia Wizara ya Madini imeanzisha program maalum ya Mining for Brighter Tomorrow (MBT) kwa lengo kusaidia vijana na wanawake kujihusisha katika uchimbaji wenye manufaa. Kuhusu Madini ya Almasi na Tanzanite Almasi: Mahitaji duniani yameshuka kutokana na ongezeko la almasi za maabara. Tanzanite: Serikali imerejesha hadhi ya madini haya kwa kutunga sheria na kurudisha masoko ya ndani. Sheria mpya inaruhusu minada ya ndani na ya kimataifa ya madini ya vito. Maudhui ya Ndani (local Content) na Ajira kwa Wazawa Ajira za moja kwa moja kwa Watanzania katika sekta ya madini zimefikia zaidi ya 16,000, huku nafasi za juu kwa baadi ya miradi mikubwa zikiwa mikononi mwa watanzania wazawa. Kampuni za Kitanzania zinashiriki moja kwa moja katika kusambaza bidhaa na huduma kwa migodi Mikubwa hali inayopelekea kunongeza ajira kwa Watanzania na mzunguko wa fedha kubaki hapa nchini.   Madini Mkakati na Muhimu kwa Teknolojia ya Kisasa Tanzania ina madini muhimu yanayotumika katika teknolojia za hali ya juu na viwanda: Kinywe (Graphite): Muhimu katika utengenezaji wa betri, hasa kwa magari ya umeme. Nikeli: Hutumika katika chuma kisichoshika kutu na betri za lithiamu-ioni. Kobalti: Hutumika kwa betri na uhifadhi wa nishati. Lithiamu: Muhimu kwa betri za magari ya umeme. Madini Adimu ya Ardhi (Rare Earth Elements REEs): Kama niobium na tantalum, yanayotumika katika simu, mitambo ya upepo, na vifaa vya kijeshi. Mkakati wa Kuongezea Thamani Madini Nchini Malengo ya 2050: Dunia inapanga kuachana na magari ya petrol na dizeli. Tanzania imejikita katika kuongeza thamani ya madini hapa nchini badala ya kuyasafirisha ghafi, ili kuboresha ajira na uchumi. Kiwanda cha Kusafisha Makinikia: Hekari zaidi ya 1300 zimetengwa Buzwagi kwa ajili ya kiwanda cha kusafisha madini, ambako Nikeli kutoka Kabanga Nickel itasafishwa. Leseni ya uchimbaji haitatolewa kwa wawekezaji ambao hawajawasilisha mpango wa kujenga kiwanda cha kusafisha madini hapa nchini, kwa mujibu wa sheria ili kulinda ajira za watanzania. Gesi ya Helium na Fursa kwa Madini ya Kinywe Tanzania ina hifadhi kubwa ya gesi ya Helium katika Songwe na Rukwa, inayotumika katika vifaa vya matibabu kama MRI. Tanzania ni ya tatu Afrika kwa uzalishaji wa Kinywe (Graphite), na mradi mkubwa unatarajiwa kuongeza uzalishaji ili kuimarisha nafasi ya nchi katika sekta hii duniani kote.Kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini 2024 Tarehe: Novemba 19-21, 2024. Mahali: Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Dar es Salaam. Mkutano huu unaleta pamoja wawekezaji, viongozi na wawaziri wa kisekta kutoka nchi mbalimbali, na maafisa kutoka nchi mbalimbali kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kukuza uwekezaji katika sekta ya madini. Kipekee, tunamshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini, mfano kampuni ya BHP inatarajiwa kurudi kuwekeza nchini kupitia mradi wa Kabanga Nickel baada ya kusitisha shughuli zake barani Afrika zaidi ya miaka 15 iliyopita.    

ALIYOYAZUNGUMZA WAZIRI WA MADINI KATIKA KIPINDI CHA GOOD MORNING CHA WASAFI TV NA RADIO Read More »

Scroll to Top